Translator

IMETOSHA

HHCTZ

BREAKING NEWS



BREAKING NEWS: Losam5 ....>>>>>>"Fashion,Entertainments,Science and Technology".......>>>>>>>Smile's Zone 5

Jumamosi, 5 Oktoba 2013

JE, UNAHITAJI KUNUNUA SIMU ILIYOTUMIKA? (SECOND HAND PHONE)


Hapa kuna mambo uanayopaswa kuzingatia kabla ya kuamua kufanya hivyo mapema kabla ya kununua simu iliyotumia kwa maneno mengine kwa lugha ya kigeni (Used Phone).
Fuatana nami katika mfululizo huu wa ulimwengu wa sayansi na teknolojia nami mwandishi wako Samuel Mwaleni wa makala hii.
Kwa kawaida watu wengi huamua kununua simu ambazo zimekwishatumika toka kwa mtu Fulani. Kwanini? Lengo ni kuepuka gharama ya simu husika, huenda kwakuwa simu hiyo dukani ni ghali sana au ni simu ulioipenda kwa muda mrefu na hukufanikiwa kuipata kwakuwa ilikuwa ni ya gharama kubwa wakati huo, huenda miaka 3 iliyopita.
Si vibaya kununua simu iliyokwishatumika toka kwa mtu fulani au hata dukani kwakuwa wapo wenye maduka ambao huuza bidhaa zilizokwisha upya wake maarufu kama mitumba. Ila waweza kuzingatia mambo yafuatayo kabla ya kununua bidhaa hizo au simu hiyo uipendayo.

 
Si vibaya kununua simu iliyokwishatumika toka kwa mtu fulani au hata dukani kwakuwa wapo wenye maduka ambao huuza bidhaa zilizokwisha upya wake maarufu kama mitumba. Ila waweza kuzingatia mambo yafuatayo kabla ya kununua bidhaa hizo au simu hiyo uipendayo.
Jambo muhimu kumbuka kuwa mwangalifu. Zaidi ya yote ni bora kununua bidhaa ikiwa mpya kwakuwa bado kuna kampuni kubwa duniani zilizo na akiba ya simu za toleo la zamani lakini bado zikiwa mpya kabisa. Kampuni kama ya Apple bado inauza simu zake za Iphone 4S na Iphone 3gs na ikiwa unahitaji unaweza kupata kwa gharama nafuu ukilinganisha na wakati zilipoingia sokoni. Kampuni ya Samsung nayo ina simu zake za Samsung Galaxy S3 .
Na jambo la kukumbuka kuwa simu nyingi kama hizo juu huenda utakapoinunua utakosa huduma mpya zinazongia sokoni kwa sasa kama iSO7 ambayo ikiwa umenunua simu aina ya Iphone 3gs huwezi kuweka mfumo huo mpya kuendesha simu yako kwa njia ya kisasa zaidi.
Kumbuka pia simu hutofautiana muundo, chunguza simu unayotaka kununua ina muundo gani. Hii inamaanisha kuwa zipo simu ambazo unaponunua hutoweza kuondoa betri yake ila tu umendaliwa sehemu maalumu unapoweza kuweka line yako ya simu na kitunza data, muziki na picha. Aina nyingine hazikuundwa uweke kitunza data, muziki na picha zako ila kitunza data kimeundwa moja kwa moja ndani ya simu. Hivyo fikiria ikiwa ni ya muda mrefu, betri ikifa utafanya nini?
Kumbuka pia huwezi kubadili mfumo wa uendeshaji wa simu zinazotumia Android OS, Window phone OS, ios au BlackBerry OS tofauti na vile watengenezaji walivyozitengeza. Hivyo kabla ya kununua jiulize: baada ya kununua utahitaji kubadilisha mfumo wake wa uendeshaji? Kumbuka ni jambo lisilowezekana hata kidogo. Na ikiwa mfumo wa uendeshaji umepitwa na wakati na simu hiyo ni toleo la miaka 3 au 4 iliyopita kuna uwezekano mkubwa kutoweza kupata huduma mpya za kisasa kwa simu hiyo kwani teknolojia inabadilika na kuwa ya kisasa siku baada ya siku.
Nunua simu kwa gharama nafuu huku ukijua ni mpya na ni toleo la karibuni angalau miaka 2 iliyopita hadi mwanzoni mwa mwaka huu.
Zipo simu za gharama nafuu na za kisasa kama Nexus 4 na Nokia Lumia 520, Samsung Galaxy Star na Samsung Galaxy Pocket ambazo ni kama 160,000/= hadi 350,000/= kwa pesa za Tanzania.
Ushauri, ni bora ununue simu kwa gharama nafuu katika maduka yanayoaminika na kupata warrant itakayokusaidia ikiwa simu uliyonunua inaleta tatizo na itakuwa rahisi kuirudisha na kurekebishiwa au kubadilishwa na kupewa nyingine. Ikiwa unanunua kwa mtu ni vyema kuifahamu simu hiyo na sababu ya yeye kuiuza, ikibidi ingia katika tovuti ya simu husika kujua ina mambo gani yanayohusika. Kwakuwa sasa kuna baadhi ya makampuni yamekuwa waigaji wazuri wa bidhaa za kampuni nyingine kwa nia ya kunufaika kupitia jina la kampuni hizo.
Jua pia alinunua lini simu hiyo, itakuwa jambo zuri kama atakupatia kitabu chake cha maelekezo ya matumizi ya simu hiyo.Baada ya hapo ndipo ufanye uamuzi wa kununua au kutonunua simu hiyo.
Pia ni muhimu kujua uhalali wa bidhaa hiyo.Imekuwa kawaida leo kwa watu kuiba simu madukani na kuziuza mtaani kwa bei nafuu.Hivyo chunguza kwa makini ikiwa bidhaa hiyo si ya wizi.
Hayo ni mambo muhimu ya kuzingatia unaponunua bidhaa zilizotumika.Tukutane wakati mwingine katika makala nyingine ya teknolojia.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni